Sunday, June 1, 2008

chachandu ya maembe mabichi

Wengi wetu tumekuwa tunahitaji sana pilipili katika kukifanya kutengeneza hamu ya kula chakula lakini tumekuwa tukishindwa kuelewa ni ipi aina bora ya pilpili kwa afya zetu .

hii hapa teknolojia rahisi ya kutengeneza pilipili kwa gharama nafuu na bila kuondoa virutubisho ambavyo ni muhimu kwa afya zetu na vilevile kati.

Mahitaji

Embe aina ya dodo bichi 1
Tangawizi 1 kubwa
Kitunguu saumu 1
Kitunguu maji 1 kikubwa
Tango 1
Pilipili hoho 1
Karoti 1 Chumvi kijiko 1 cha chakula
Nyanya nne kubwa
Pilipili mbuzi za kuiva 10
vinega

Namna ya kutengeneza.

Chukua vitu vyote viweke kwenye bakuli kubwa la plastiki na osha kwa kutumia maji ya moto ili kuhakikisha usafi zaidi .

Menya embe pamoja na viungo vingine vinavyotakiwa kumenywa kisha katakata katika vipande vidogovidogo halafu weka katika mashine ya kusagia na uvisage hadi viwe kama uji mzito .

Hifadhi katika chupa tayari kwa kuliwa ,waweza kula na vyakula kama wali.ndizi au waweza kula kama achali kwa kula na bagia au kababu.

No comments:

Post a Comment