Sunday, June 1, 2008

Chatini Ya Ukwaju

Chatini ya ukwaju ni mchanganyiko ambao umebuniwa kwa ufundi mkubwa kwani una harufu na ladha ya kuvutia na hii yote ni katika kufanya chakula kiwe na ladha na hata thamani zaidi .
Ukwaju ni kiungo ambacho ambacho kwa watu wengi wamekuwa wakitumia kama juice tu lakini ni kiungo chenye matumizi mengi kuliko watu wanavyofikiria .

Kwa watu wa pwani hasa katika visiwa vya unguja na pemba ukwaju umekuwa ukitumika kama ndimu katika chakula kwa lengo la kuchangamsha chakula husika.
Vilevile ukwaju umekuwa ukitumika kama vinega kwa kutumika kwenye saladi na mara nyingine hutumika kwenye vyakula vyenye shombo kwa lengo la kukata shombo.

mahitaji
UkwajuTangawizi mbichiPilipili mbichi kiasi unachohitajiKitunguu Saumu kitunguu maji ( si lazima vile )chumvi
(Vipimo itategemea kiasi unachohitaji)

Namna ya kutengeneza

Anza kwa kutwanga vitunguu maji na swaumu.
Changanya na pilipili halafu huku ukiendelea kutwanga hadi vilainike .
Weka chumvi kiasi
Chukua ukwaju menya maganda yake na kamua na kupata rojo nzito .
Changaya pamoja na mchanganyiko huo uliotwanga .
Mpaka hapo chatini yako itakuwa tayari kwa kuliwa waweza kutumia katika chipsi katres pamoja na vitafunwa vingine au waweza kutumia katika mlo kama wali na ugali.

No comments:

Post a Comment