Wednesday, October 10, 2012

Jokate Mwegelo azindua kampuni ya nywele




 My People,Jokate Mwegelo posing with William Malecela at Serena
 My People,Jokate Mwegelo posing with William Malecela at Serena
Johnson Lujwangana posing with William Malecela a.k.a Big Show
 Ohhh
 They love kabelelejr blog
 Bro William Malecela posing with Meneja Masoko wa Kampuni ya Kidoti Peter Kasiga
 They look poa sanaaaa
 Sinta a.k.a JLO wa Bongo,the one and only Christina.Nywele by KIDOTI
 We Sinta wewe....Mbona umependeza sanaaaaaaa
 OMG......umeuwa wangu,kudadadekiiiiiiiii
 Nikaona ngoja nikuvute kama siyo ku-ZOOM huo mkoba,umetokelezea ile mbayaaaa
 Mgongo unao,sijabisha hata kidogo mamiiiiiiii
 Kumbe hata mguu unalipa...safiiiiiii
 Hiyo rangiya kucha tuuuu,maana
 Mpaka Big Boss William akaona hapana,ngoja na yeye afanye kweliiiii hahahaha
 Nawakubali sanaaaaaaaaaaaaaaaaa
 Weraaaaaaaaa,SINTA;SEIF KABELELE;ESI and WILLIAM MALECELA
 PARTYY PEOPLEEEEE
 Oh yesssssssssssss,Kabelele,Sinta,Esi and MalecelaJr
 Dats what am talking about yoooo
 BBM ilihusu
 Unabisha_
 I love them jamani,Bea,Sinta and Jokate
 Me love you long time wadada
 I love u mingimingi mnoooooooo
 Oh Goshhhh
 I like dat Jokate
 Bro William umetishaaaaaaaaaaaaa
 Wen em Tz New Yorkers meet hahahahahaa,Bea and Le Mutuz a.k.a William
Meneja Masoko wa Kampuni ya Kidoti Peter Kasiga pamoja na CEO wa Kidoti Jokate Mwegelo wakijibu maswali kwa waandishi wa habari wakati wa uzinduzi huo ambapo pia amefafanua kuzinduliwa rasmi kwa tovuti ya kampuni hiyo leo itakayopatikana kupitia anuani ya www.kidotiloving.com
Kidoti ambayo ni chapa halisi ya Kitanzania imezinduliwa rasmi leo jijini Dar es Salaam.
Chapa ya Kidoti imeundwa katika taswira yake mwenyewe Jokate.
Sifa zake alizohakikisha zinaonekana kupitia Kidoti ni pamoja na akili, ujasiri, dhamira, yenye kuthubutu lakini pia yenye bashasha zote za kike.
Kidoti haitaishia katika mavazi na mitindo tu.
Kidoti ni harakati na mwanzo wa chapa ya mitindo-maisha yenye nia kuu ya kuwezesha kizazi change,” aliongeza Jokate.
Nywele sanisi za Kidoti ambazo zimezinduliwa leo katika soko ni zenye ubora wa hali ya juu zikiwa zimejaribiwa na wateja wake watarajiwa wenyewe.
Mtiririko mzima wa ubunifu na uzalishaji wa bidhaa hizi ulisimamiwa na kuongozwa na Jokate ambapo kila nywele zimejaribiwa na kukidhi matakwa ya kudumu, kuweza kutumiwa tena na tena, uzito pamoja na msokotano.
Nywele hizi zinakuja katika mitindo na urefu mbalimbali ambayo imebeba sifa za chapa hii zikiwa na mawimbo nyororo kwa ajili ya wanawake wanaopenda kupendeza bila kufilisi mifuko yao.
Pamoja na ubora wake wa hali ya juu, nywele hizi zinaendana kabisa na nia ya Kidoti ya kuvuruga na kuleta maana mpya katika tasnia ya mitindo kwa ubunifu wa kuweza kutengeneza mitindo mingi kutumia nywele moja na sifa hii inawasilishwa kwa soko walengwa kibunifu kupitia kasha za bidhaa hizi ambazo zimesheheni picha za Jokate mwenyewe akionyesha mitindo mbalimbali kwa ajili ya kila nywele. Sifa hii ya kipekee pia inawasilishwa kupitia maneno “nywele moja staili kibao!” yaliyochapishwa katika kila kasha.
Nywele za Kidoti zitapatikana kwa bei nafuu kupitia mawakala mbalimbali wa jumla na rejareja jijini kuanzia leo na zitauzwa kwa kati ya Sh. 9,500 na 12,000.
Mawakala hawa ni pamoja na maduka ya jumla na rejareja Kariakoo, saluni mbalimbali jijini na mtandao wa mawakala mikoani utakaokuwa na bidhaa zetu kuanzia wiki ijayo.
Nguo za Kidoti zitatambulishwa rasmi katika soko mwakani (2013) zikifuatiwa na vifuasi vya urembo pamoja na vipodozi.
Harakati ya Kidoti inaendeshwa na timu ya vijana wabunifu pamoja na kwamba shughuli za Kidoti zinaendeshwa kutoka Dar es Salaam, chapa hii ni ya kiulimwengu zaidi.
Chapa ya Kidoti ilianzishwa mwaka 2011 na Bi. Jokate Mwegelo ambaye ni mmoja wa watu mashuhuri nchini, kwa nia ya kubadilisha mtazamo mzima wa tasnia ya mitindo. Chapa hii itasheheni bidhaa mbalimbali zikiwemo nywele za sanisi ambazo zimezinduliwa leo pamoja na chapa. Bidhaa nyinginezo ni pamoja na nguo, vifuasi vya urembo pamoja na vipodozi.
Kidoti ni chapa yenye uwezo wa kubadilisha jinsi tunavyoichukulia tasnia ya mitindo hivi sasa.

Story kwa hisani ya SEIF KABELELE

No comments:

Post a Comment