Saturday, August 21, 2010

Kanga jeans katika ulimwengu wa fashion

Katika kuhakikisha anaitangaza vizuri nchi yake. Mbunifu wa mitindo wa kitanzania Vida Mahimbo amekuja na Collection mpya kabisa inayofahamika kama Kanga Jeans.

Kanga jeans kwa mara ya kwanza kabisa ilionyeshwa katika New york Fashion week. Ambapo wadau wengi walionyesha kuikubali collection hiyo.

Kwa kuwa Lengo lake ni kuisambaza dunia nzima. Tarehe 11 ya mwezi huu, Vida mahimbo alionyesha vitu vyake hivyo katika ufukwe Forte Dei Marmi nchini Italia.
Hivi sasa anaazimia kuonyesha ubunifu wake huo nchini. Na kwa kuanzia ataonyesha katika fukwe za Zanzibar . Hapo wadau wa mitindo watapata wasaa wa kujionjea ladha ya mavazi yake hayo.

No comments:

Post a Comment