Monday, August 24, 2009

Stefanía Fernández miss Universe 2009

Mrembo Stefania Fernández (18) ambaye ni Miss Venezuela amejinyakulia taji la miss Universe kwa mwaka 2009 shindano lililofanyika kisiwa cha Atlantis Paradise kilichopo Nassau, Bahamas.


Nafasi ya pili imeenda kwa Miss Dominican Republic Ada de la Cruz na ya tatu imekamatwa naye Miss Kosovo Marigona Dragusha.

Shindano hilo lilifanyika jana August 23, 2009 ikiwa ni mara ya 58 tangu kuanzishwa kwake, ambapo nchi 84 duniani zilishiriki Tanzania ikiwa mmoja wapo.
Mwakilishi wa Tanzania Illuminata Wize, ameambulia patupu kwani hakuweza hata kuingia kumi na tano bora.

Nchi zilizoingia kumi na tano bora ni pamoja na Albania, Australia, Ubelgiji Croatia, Jamuhuri ya Czech,Jamuhuri ya Dominican, Ufaransa, Iceland, Kosovo, Puerto Rico, Sweden, Switzerland, South Africa, Marekani na Venezuela.

Hii ni mara ya pili mfululizo taji hilo kwenda nchini venezueala ambapo mwaka jana lilichukuliwa na Dayana Mendoza kutoka nchi hiyo

No comments:

Post a Comment