Sunday, June 1, 2008

Kamba wa nazi




mahitaji


kamba wabichi 10 mafuta ya kula vijiko 4 vya mezanikitunguu maji 1 tangawizi mbichi iliyosagwa kijiko 1 cha mezanikitunguu saumu kilichosagwa kijiko1 cha chaibinzari ¼ kijiko cha chaiunga wa pilipili ¼ kijiko cha chaikotmiri iliyokatwakatwa kijiko 1 cha mezani.pilipil hoho 1 tui la nazi kikombe cha chai 1limao au ndimu 1.

Namna ya kutengeneza


Menya kamba wako kisha waweke pembeni. chukua kikaango anza kukaanga kitunguu maji,kisha weka saumu na tangawizi endelea kukaanga hadi viwe hudhurungi.kisha weka binzari na unga wa pilipili halafu kotmiri.
Weka maji kidogo ykianza kuchemka weka kamba wako acha wachemke kwa dakika 3 hadi 4 punguza moto kidogo ili viive kwa nafasi.
Baada ya hapo miminia tui la nazi baada ya kuchemka na kupata kiasi cha mchuzi unachohitaji weka kamulia limao au ndimu kisha chumvi.
Kamba wako tayari kwa kuliwa waweza kula na wali ugali au kitafunwa chochote.
Huu ni mlo kwa ajili ya watu wawili.

No comments:

Post a Comment