Saturday, May 31, 2008

krispy za mbatata



Viazi mbatata ama ulaya kama watu wengi wanavyopendelea kuviita ni kati ya chakula kilicho na mapishi mengi kama vile mchele.

Na mara nyingi vyakula hivyo hutofautina kwa majina kutokana na namna vinavyotengenezwa nah ii ni kutokana na usanii unaofanywa na wapishi katika kukamilisha sanaa hii muhimu.

Krisp ni moja kati ya upishi mmojawapo unaotokana na viazi mbatata, lakini je unajua zinatengenezwaje?

Mahitaji Viazi mbatata kiasi. Chumvi kiasi. Mafuta ya kupikia ya maji. Mashine ya kuparuzia karoti (grating machine) Namna ya kupika Menya viazi vyako , kisha vioshe vizuri.Hakikisha hauuachi na majimaji Unahitaji kuwa na kile kimashine kidogo cha kuparuzia nyanya au karoti(grating machine) au kama huna waweza kutumia kisu kukatakata katika maduara membamba
Vianike kidogo viwe vikavu. weka mafuta, wacha yapate moto. Vimimine ndani ya mafuta, uvikaange
Geuzagauza visishikane. Wacha mpaka viwe rangi ya hudhurungi
Ipua nyunyuzia chumvi , wacha vipoe.Tayari kwa kuliwa

No comments:

Post a Comment